- Joined
- Jun 4, 2023
- Messages
- 7,628
- Reaction score
- 26,450
- Points
- 113
Kifo ni fumbo kubwa sana kwa mwanadamu japo wako wengi waliojaribu kufumbua fumbo la kifo wameshindwa. Hata wanasayansi wakiobobea wamejaribu kutengeneza maisha ya Kudumu ila kifo kikawaita.
Hapa kupitia uzi huu tutawakumbuka ndugu zetu au marafiki zetu waliotangulia mbele za haki kwa kuwapa salamu za upendo na kishea kumbukumbu zao na wanakijiji wenzetu
Napenda kumkumbuka Ruby
Kuna msichana nilisoma nae shule ya msingi anaitwa Ruby. Ni ndugu yake muigizaji wa bongo movie Thea. Tulipenda sana kucheza nae mpira wa miguu na alipenda sana kutubutua na mpira wa kufuma
Tukiwa darasa la tano Ruby alipatwa na kansa ya mguu tena ule mguu aliopenda kupigia mpira. Akiwa anapata matibabu ocean road walilazimika kumkata mguu. Ruby msichana mdogo wa umri wa miaka 10 tu akawa na mguu mmoja
Baadae tena taarifa ikaja kuwa kansa imeamia mguu wa pili. Hapo hata kidonda cha mguu wa kwanza hakijapona. Sitasahau siku ile nilivyomuona mara ya mwisho akiwa mweupe sana kwa kukaa ndani mda mrefu. Tulishiriki maombi ya pamoja sikuwaza kuwa haya yangekuwa maombi yetu ya mwisho pamoja
Siku chache baadae rafiki yangu Ruby alifariki na akazikwa makaburi ya Kinondoni. Nimekuwa nikimkumbuka sana Ruby na nimemtafuta Thea zaidi ya mara moja kumuomba picha ya Ruby hata nipate kuwa na kumbukumbu ya picha yake bila mafanikio.
Ujumbe wangu kwa Ruby ni kuwa bado namkumbuka. Ingawa ametutoka bado hajanitoka moyoni mwangu. Nakukumbuka sana Ruby. Ningependa siku moja tuonane tena huko Sayuni. Najua nikifa leo moja kwa moja motoni ila nitafahya jitihada kuishi vyema tuwe pamoja karamuni. .
Napenda kumkumbuka Paulo
Maisha ya ulimwengu huu hayajawahi kuwa ya haki. Kifo kilimchukua rafiki yangu mpendwa Paulo. Hata sijawahi ona kaburi lake wala kumuaga safari yake ya mwisho.
Kwa miaka hiyo huyu rafiki yangu alizaliwa afe. Hakuwahi kufurahia matunda ya maisha ya duniani..Akiwa mdogo alipoteza wazazi wake wote kwa gonjwa hatari la UKIMWI. Kipindi hicho ulikuwa unaitwa miwaya au umeme.
Nimepoteza baadhi ya watu kwa gonjwa hili ila Paulo hakupata haki. Alipata UKIMWI kutoka kwa wazazi wake. Hata wazazi wake walifariki mapema bila hata kuwa na kumbukumbu nzuri juu ya wazazi wake.
Maisha ya Paulo yalikuwa ya kuumwa umwa kila wakati. Hakuweza kucheza vizuri na watoto wa rika lake. Mtaani wazazi walizuia watoto wao kucheza na Paulo. Hakika rafiki yangu huyu alitengwa na jamii. Alifariki akiwa na miaka 11 sikuweza hata kumuaga rafiki yangu huyu.
Natumaini iko siku nitapata kumuona tena Paulo na kucheza nae michezo ya utotoni. Hakuweza kufaidi kucheza na watoto wezake. Najua Paulo amekufa kifo chema akiwa na upako wa mwisho. Endelea kupumzika kwa amani Paulo. .
Hapa kupitia uzi huu tutawakumbuka ndugu zetu au marafiki zetu waliotangulia mbele za haki kwa kuwapa salamu za upendo na kishea kumbukumbu zao na wanakijiji wenzetu
Napenda kumkumbuka Ruby
Kuna msichana nilisoma nae shule ya msingi anaitwa Ruby. Ni ndugu yake muigizaji wa bongo movie Thea. Tulipenda sana kucheza nae mpira wa miguu na alipenda sana kutubutua na mpira wa kufuma
Tukiwa darasa la tano Ruby alipatwa na kansa ya mguu tena ule mguu aliopenda kupigia mpira. Akiwa anapata matibabu ocean road walilazimika kumkata mguu. Ruby msichana mdogo wa umri wa miaka 10 tu akawa na mguu mmoja
Baadae tena taarifa ikaja kuwa kansa imeamia mguu wa pili. Hapo hata kidonda cha mguu wa kwanza hakijapona. Sitasahau siku ile nilivyomuona mara ya mwisho akiwa mweupe sana kwa kukaa ndani mda mrefu. Tulishiriki maombi ya pamoja sikuwaza kuwa haya yangekuwa maombi yetu ya mwisho pamoja
Siku chache baadae rafiki yangu Ruby alifariki na akazikwa makaburi ya Kinondoni. Nimekuwa nikimkumbuka sana Ruby na nimemtafuta Thea zaidi ya mara moja kumuomba picha ya Ruby hata nipate kuwa na kumbukumbu ya picha yake bila mafanikio.
Ujumbe wangu kwa Ruby ni kuwa bado namkumbuka. Ingawa ametutoka bado hajanitoka moyoni mwangu. Nakukumbuka sana Ruby. Ningependa siku moja tuonane tena huko Sayuni. Najua nikifa leo moja kwa moja motoni ila nitafahya jitihada kuishi vyema tuwe pamoja karamuni. .
Napenda kumkumbuka Paulo
Maisha ya ulimwengu huu hayajawahi kuwa ya haki. Kifo kilimchukua rafiki yangu mpendwa Paulo. Hata sijawahi ona kaburi lake wala kumuaga safari yake ya mwisho.
Kwa miaka hiyo huyu rafiki yangu alizaliwa afe. Hakuwahi kufurahia matunda ya maisha ya duniani..Akiwa mdogo alipoteza wazazi wake wote kwa gonjwa hatari la UKIMWI. Kipindi hicho ulikuwa unaitwa miwaya au umeme.
Nimepoteza baadhi ya watu kwa gonjwa hili ila Paulo hakupata haki. Alipata UKIMWI kutoka kwa wazazi wake. Hata wazazi wake walifariki mapema bila hata kuwa na kumbukumbu nzuri juu ya wazazi wake.
Maisha ya Paulo yalikuwa ya kuumwa umwa kila wakati. Hakuweza kucheza vizuri na watoto wa rika lake. Mtaani wazazi walizuia watoto wao kucheza na Paulo. Hakika rafiki yangu huyu alitengwa na jamii. Alifariki akiwa na miaka 11 sikuweza hata kumuaga rafiki yangu huyu.
Natumaini iko siku nitapata kumuona tena Paulo na kucheza nae michezo ya utotoni. Hakuweza kufaidi kucheza na watoto wezake. Najua Paulo amekufa kifo chema akiwa na upako wa mwisho. Endelea kupumzika kwa amani Paulo. .