- Jun 4, 2023
- 7,020
- 22,618
- 113
Mbeya. Siku moja baada ya mwanafunzi, Esther Noah kupatikana akiwa hai, anaendelea na vipimo kwenye Hospitali ya Rufaa kitengo cha Wazazi Meta jijini Mbeya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Mwanafunzi huyo (18) wa kidato cha tano katika shule ya sekondari Panda Hill alidaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha tangu Mei 18 mwaka huu na jana Juni 23 alipatikana akiwa hai.
Esther alikutwa mtaa wa Ifisi mji mdogo wa Mbalizi mkoani Mbeya akiwa kwenye nyumba ya mfanyabiashara wa mkaa aitwaye Azurath Mohamed ambaye alieleza kukabidhiwa na mteja wake aliyejulikana kwa jina la Baba Jose.
Akizungumza na Mwananchi Digital, leo Jumamosi June 24, 2023, mama mdogo na mlezi wa mwanafunzi huyo, Happy Yobi amesema kwa sasa wapo hospitali ya Meta kwa matibabu zaidi baada ya kufika nyumbani usiku wa kuamkia leo Jumamosi, Juni 24.
Amesema hali yake si mbaya akibainisha kuwa ishu ya usalama ni ya kawaida kwani nyumbani kwao mtaa wa Forest nyumba waliyopo ina kila kitu ndani hivyo hawana wasiwasi sana.
“Tunaishi naye kwa tahadhari na umakini japokuwa nyumba ina kila kitu ndani hawezi kupotea, tulifika usiku na leo tupo hospitali hapa Meta kwa matibabu zaidi,”
“Ni mapema sana kuzungumza naye kila kitu, tumeamua asiongee chochote apumzike kwanza kwa sababu vyombo vya dora vilimuhoji kila kitu hivyo tuwaachie wao, mimi na mume wangu ndio tulimlea akiwa na miaka miwili hadi sasa,” amesema Happy.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo, Zephania James amesema wanaendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi akieleza kuwa mwanafunzi huyo alikuwa mpenda michezo na hakuwa na tabia mbaya zaidi.
“Alikuwa mtu wa kawaida anapenda kujichanganya na wenzake na alipendelea zaidi michezo, nidhamu yake ilikuwa nzuri na sijawahi kupata taarifa mbaya kutoka kwake,” amesema James.
MWANANCHI
Mwanafunzi huyo (18) wa kidato cha tano katika shule ya sekondari Panda Hill alidaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha tangu Mei 18 mwaka huu na jana Juni 23 alipatikana akiwa hai.
Esther alikutwa mtaa wa Ifisi mji mdogo wa Mbalizi mkoani Mbeya akiwa kwenye nyumba ya mfanyabiashara wa mkaa aitwaye Azurath Mohamed ambaye alieleza kukabidhiwa na mteja wake aliyejulikana kwa jina la Baba Jose.
Akizungumza na Mwananchi Digital, leo Jumamosi June 24, 2023, mama mdogo na mlezi wa mwanafunzi huyo, Happy Yobi amesema kwa sasa wapo hospitali ya Meta kwa matibabu zaidi baada ya kufika nyumbani usiku wa kuamkia leo Jumamosi, Juni 24.
Amesema hali yake si mbaya akibainisha kuwa ishu ya usalama ni ya kawaida kwani nyumbani kwao mtaa wa Forest nyumba waliyopo ina kila kitu ndani hivyo hawana wasiwasi sana.
“Tunaishi naye kwa tahadhari na umakini japokuwa nyumba ina kila kitu ndani hawezi kupotea, tulifika usiku na leo tupo hospitali hapa Meta kwa matibabu zaidi,”
“Ni mapema sana kuzungumza naye kila kitu, tumeamua asiongee chochote apumzike kwanza kwa sababu vyombo vya dora vilimuhoji kila kitu hivyo tuwaachie wao, mimi na mume wangu ndio tulimlea akiwa na miaka miwili hadi sasa,” amesema Happy.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo, Zephania James amesema wanaendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi akieleza kuwa mwanafunzi huyo alikuwa mpenda michezo na hakuwa na tabia mbaya zaidi.
“Alikuwa mtu wa kawaida anapenda kujichanganya na wenzake na alipendelea zaidi michezo, nidhamu yake ilikuwa nzuri na sijawahi kupata taarifa mbaya kutoka kwake,” amesema James.
MWANANCHI