- Jul 9, 2023
- 3,787
- 3,778
- 113
Mapendekezo ya wafanyabiashara
Kasi ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Wafanyabiashara kwa sababu kuna mambo mengi mazuri yanayoweza kustawisha biashara na sekta binafsi. Serikali inatakiwa kutochoka kukutana na wafanyabiashara mara kwa mara, kwa sababu wao ndio wanajua shida zinazowakabili.
Kuipa kipaumbele sekta binafsi
Sekta binafsi inayomilikiwa na Watanzania kupewa kipaumbele kwenye zabuni hususani kwenye ujenzi kwa sababu asilimia kubwa ya bajeti ya Tanzania huishia kwenye ujenzi lakini wanufaika wakubwa wa hizo zabuni ni kampuni za nje, hii inadhoofisha ukuaji wa sekta binafsi ya Watanzania.
Kuweka kodi rafiki
Kuendelea kupunguza tozo na kodi mbalimbali ili Wafanyabiashara waweze kuvutiwa kufanya biashara. Pia ni muhimu kuendelea kutoza kodi kubwa bidhaa zinazotoka nje ili zinazozalishwa ndani zipate soko na kukuza sekta binafsi.
Mzunguko wa fedha
Ni muhimu kuongeza ujazo wa fedha katika mzunguko kiuchumi, hili anaweza kulitekeleza kwa kuanza kulipa madeni ya watu wenye kandarasi mbalimbali serikalini ambao bado hawajalipwa stahiki zao.
Karibuni kutoa maoni mbalimbali jinsi ya kukuza uchumi wa Tanzania.
Kasi ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Wafanyabiashara kwa sababu kuna mambo mengi mazuri yanayoweza kustawisha biashara na sekta binafsi. Serikali inatakiwa kutochoka kukutana na wafanyabiashara mara kwa mara, kwa sababu wao ndio wanajua shida zinazowakabili.
Kuipa kipaumbele sekta binafsi
Sekta binafsi inayomilikiwa na Watanzania kupewa kipaumbele kwenye zabuni hususani kwenye ujenzi kwa sababu asilimia kubwa ya bajeti ya Tanzania huishia kwenye ujenzi lakini wanufaika wakubwa wa hizo zabuni ni kampuni za nje, hii inadhoofisha ukuaji wa sekta binafsi ya Watanzania.
Kuweka kodi rafiki
Kuendelea kupunguza tozo na kodi mbalimbali ili Wafanyabiashara waweze kuvutiwa kufanya biashara. Pia ni muhimu kuendelea kutoza kodi kubwa bidhaa zinazotoka nje ili zinazozalishwa ndani zipate soko na kukuza sekta binafsi.
Mzunguko wa fedha
Ni muhimu kuongeza ujazo wa fedha katika mzunguko kiuchumi, hili anaweza kulitekeleza kwa kuanza kulipa madeni ya watu wenye kandarasi mbalimbali serikalini ambao bado hawajalipwa stahiki zao.
Karibuni kutoa maoni mbalimbali jinsi ya kukuza uchumi wa Tanzania.