mshamba_mkuu
New member
- Jun 4, 2023
- 1,563
- 4,525
- 0
Umeshawahi kukumbuka kitu, kwenda mahali, kuona kitu, kugusa kitu, kunusa kitu au hata kuambiwa kitu, halafu ukakumbuka kitu flani cha zamani kwenye maisha yako, ukapata hisia flani ambayo ni kama mchanganyiko wa furaha, huzuni na shauku?? Hii hisia inaitwa nostalgia
Nostalgia ni hisia ya raha na wakati mwingine huzuni kidogo wakati huo huo unapofikiria juu ya mambo yaliyotokea zamani.... Mimi nimejikuta napenda sana kupata hii hisia, kukumbukia vitu vya zamani inanipa amani flani moyoni. Vitu vinavyonipa nostalgia ni kama;
-nikiwa maeneo ya shule nilizosoma hapo awali
-filamu au miziki niliyoipenda sana zamani au hata nikiwa mtoto kabisa
-watu ambao ulikua nao karibu zamani ila mkapotezana afu mkakutana sasa
-picha mbalimbali ulizopiga kwenye matukio ya zamani
-vyakula na vinywaji ambavyo unakua hujavitumia kwa mda mrefu sana
-mahali flani maalum ambapo pana umuhimu kwako mfano; nyumbani kwa bibi, kaburi la mtu wako wa karibu
-na vitu vingine mbalimbali kama vitabu, simu ulizotumia zamani.... mfano; kuna kitabu cha hadithi nilikua nakipenda sana nikiwa mdogo nikaja kukipata tena hivi karibuni nilipokifungua nikawa napata kumbukumbu nyingi za kipindi hicho, kumbukumbu ambazo hata nilikua sijui kama bado ninazo
ndio maana kukusanya kumbukumbu za matukio mbalimbali kwenye hatua mbalimbali za maisha yako inaweza ikawa na muhimu, ile hisia unayoipata wakati unarudisha matukio nyuma kwenye akili yako inakuonyesha mapito mbalimbali uliyopitia mpaka kufikia hapo ulipo....
Je na wewe unapata nostalgia?? vitu gani hasa vinakukumbusha mbali??
Nostalgia ni hisia ya raha na wakati mwingine huzuni kidogo wakati huo huo unapofikiria juu ya mambo yaliyotokea zamani.... Mimi nimejikuta napenda sana kupata hii hisia, kukumbukia vitu vya zamani inanipa amani flani moyoni. Vitu vinavyonipa nostalgia ni kama;
-nikiwa maeneo ya shule nilizosoma hapo awali
-filamu au miziki niliyoipenda sana zamani au hata nikiwa mtoto kabisa
-watu ambao ulikua nao karibu zamani ila mkapotezana afu mkakutana sasa
-picha mbalimbali ulizopiga kwenye matukio ya zamani
-vyakula na vinywaji ambavyo unakua hujavitumia kwa mda mrefu sana
-mahali flani maalum ambapo pana umuhimu kwako mfano; nyumbani kwa bibi, kaburi la mtu wako wa karibu
-na vitu vingine mbalimbali kama vitabu, simu ulizotumia zamani.... mfano; kuna kitabu cha hadithi nilikua nakipenda sana nikiwa mdogo nikaja kukipata tena hivi karibuni nilipokifungua nikawa napata kumbukumbu nyingi za kipindi hicho, kumbukumbu ambazo hata nilikua sijui kama bado ninazo
ndio maana kukusanya kumbukumbu za matukio mbalimbali kwenye hatua mbalimbali za maisha yako inaweza ikawa na muhimu, ile hisia unayoipata wakati unarudisha matukio nyuma kwenye akili yako inakuonyesha mapito mbalimbali uliyopitia mpaka kufikia hapo ulipo....
Je na wewe unapata nostalgia?? vitu gani hasa vinakukumbusha mbali??
Last edited by a moderator: