Diet Plan for pregnant woman

Gily

KF Founder & Dragon IGM
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 4, 2023
Messages
7,590
Reaction score
26,196
Points
113
Wasalaam
Wakati wife yuko pregnant alipenda kula sana mapapai. Hii ilimpelekea shida kwa sababu chupu chupu mimba itoke. Hakuna kati yetu aliyejua kuwa mapapai yanaweza kusababisha mimba kutoka yakizidi.

Hivyo basi hapa kutakuwa na mchango wa mawazo mbali mbali juu ya vyakula salama kwa wamama wajawazoto. Je wewe au mkeo ulikuwa na ratiba ipi ya chakula ambayo ni nzuri kwa ukuaji wa mtoto tumboni na salama kwa mama mjamzito?
 
tuambie kwanza wewe na mkeo ratiba yenu ilikuaje,,ukiachana na hayo mapapai😊
Yeye alikuw anahakikisha kuna mboga za majani kwenye kila mlo. Ana tatizo la kupungua damu akiwa mjamzito hivyo alikuwa anajutahidi anapata vitamin c pamoja na mboga za majani kwa wingi.
 
Yeye alikuw anahakikisha kuna mboga za majani kwenye kila mlo. Ana tatizo la kupungua damu akiwa mjamzito hivyo alikuwa anajutahidi anapata vitamin c pamoja na mboga za majani kwa wingi.
okay vizuri,,,unaweza kuniambia pia vyakula gani inatakiwa asivitumie kwenye hicho kipindi cha ujauzito...nachukua experience kutoka kwenu😊
 
okay vizuri,,,unaweza kuniambia pia vyakula gani inatakiwa asivitumie kwenye hicho kipindi cha ujauzito...nachukua experience kutoka kwenu😊
Kuna baadhi ya vyakula nadhan si vizuri sana kwa wajawazito. Mfano protein ikizidi mtoto akanenepa sana kutakuwa na shida ya kujifungua.
 
Aseme kwa kweli 😂
Kwanza nilihakikisha kwenye kila chakula anapata mboga za majani na matunda. Kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa kupata choo kigumu kwa wajawazito

Pili nilihakikisha anakuwa na maji safi na salama karibu. Hii ni kutokana na kuwa wanatakiwa wawe hydrated mda wote

Tatu anakula vyakula tofauti tofauti ili apate lishe tofauti. Kulikuwa na ratiba ya vyakula kwa wiki ina maana kila siku alipata chakula tofauti

Nne, nilijitahidi afanye mazoezi baada ya kula ili kusaidia chakula kumengenywa vizuri. Wakati mwingine ukila unapata uchovu mwingi na kulala. Hivyo mazoezi madogo madogo husaidia asipate kiungulia

Tano, nilihakikisha anapewa dawa za minyoo clinic ili chakula kisiwe kinapotea bure mwilini kwa afya ya mama na mtoto.
 
Kwanza nilihakikisha kwenye kila chakula anapata mboga za majani na matunda. Kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa kupata choo kigumu kwa wajawazito

Pili nilihakikisha anakuwa na maji safi na salama karibu. Hii ni kutokana na kuwa wanatakiwa wawe hydrated mda wote

Tatu anakula vyakula tofauti tofauti ili apate lishe tofauti. Kulikuwa na ratiba ya vyakula kwa wiki ina maana kila siku alipata chakula tofauti

Nne, nilijitahidi afanye mazoezi baada ya kula ili kusaidia chakula kumengenywa vizuri. Wakati mwingine ukila unapata uchovu mwingi na kulala. Hivyo mazoezi madogo madogo husaidia asipate kiungulia

Tano, nilihakikisha anapewa dawa za minyoo clinic ili chakula kisiwe kinapotea bure mwilini kwa afya ya mama na mtoto.
Dawa za minyoo mara kwa mara ?
 
Back
Top