Faida za kushangaza ambazo pengine hukuzijua za kutumia papai

Hakimu

Immortal Village Hero
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 3, 2023
Messages
2,714
Reaction score
6,233
Points
113
Papai ni tunda la kushangaza na lenye afya. Ina 'antioxidants' ambayo hupunguza kuvimba na kupambana na magonjwa na kusaidia mtu kuonekana na umri mdogo.

1690042098950.png

Virutubisho katika papai​

Kalori, Wanga, Nyuzinyuzi, Protini, Vitamini C, Vitamini A, Vitamini B9, Potasiamu, Kalsiamu na Magnesiamu.

Faida za kiafya za Papai​

Huzuia Saratani : Utafiti unaonyesha kuwa 'lycopene' iliyomo kwenye papai inaweza kupunguza hatari ya saratani. Inaweza pia kuwa muhimu kwa watu wanaopata matibabu ya saratani.
Papai lina wingi wa vitu vya kuzuia saratani ikiwa ni pamoja na folate, vitamini C, beta-carotene na vitamini E ambayo hupunguza hatari ya saratani.

Utafiti mdogo uliofanywa kwa watu wazima wenye kuvimba na shida ya tumbo, ulipunguza madhara ya msongo na seli za saratani. Hata hivyo, utafiti zaidi unahitajika kabla ya kufikia hitimisho.
Cholesterol na Afya ya Moyo: Tafiti zimeonyesha kuwa matunda na mbomboga zenye 'lycopene na Vitamin C zinaweza kuzuia magonjwa ya moyo. Antioxidants zinazopatikana kwenye papai hulinda mishipa ya moyo dhidi ya kuziba kwa cholesterol na kusababisha mshtuko wa moyo.
Gesi na Ukosefu wa Chakula: Papai hupunguza asidi tumboni, ikiwa mtu ana kiungulia na maumivu ya tumbo, papai ni tiba. Papai pia ni tiba ya shida ya kukosa kusaga chakula, colic na colic.

Afya ya Ngozi na Nywele: Papai hung'arisha ngozi na kukuza nywele kutokana na wingi wa vitamin A iliyomo na kuamsha tezi za mafuta mwilini na nywele, pia papai hupunguza chunusi ndio maana baadhi ya makampuni hupendekeza soko la mfuta 'krimu' au losheni za ngozi zao ambazo zimetengenezwa au zenye papai.
Maumivu ya hedhi: Papai ni miongoni mwa vyakula vinavyotumika kwa maumivu wakati wa hedhi, kwa vile papai huwa na kitu kinachojulikana kwa jina la "papain" ambacho kinahusiana na damu ya hedhi, imeonekana kuchangia katika kurekebisha na kuboresha hali.
Mtoto wa jicho: Papai imeonekana kupunguza hatari ya mtoto wa jicho. Papai lina wingi wa Vitamin A na beta-carotene ambazo ni muhimu kwa afya ya macho na uwezo wa kuona. Papai na karoti ni vyakula viwili ambavyo vimekubaliwa kuyapa macho afya kamili.
Pumu: Papai ni moja ya vyakula vinavyopunguza hatari ya pumu kwa sababu lina beta-carotene nyingi. Ikiwa una pumu, jaribu kula papai.
Afya ya Mifupa: Papai huongeza ufyonzaji wa kalsiamu kutoka kwenye mifupa, hupunguza utolewaji wa kalsiamu na figo, na huwa na protini zinazolinda mifupa, ambazo zote kwa pamoja husababisha mifupa yenye afya.


BBC SWAHILI
 
Kwenye ngozi nakubali hata lotion yenye papai huwa nzuri mno
 
papai liwe lekundu ilo la nyano hapana
 

Similar threads

Matunda mengi yana manufaa lakini tango linaonekana kutia fora kwa manufaa katika mwili wa binadamu. Kutokana na faida za Tango, unashauriwa kula tango kila siku, utaona manufaa yake. Kupunguza hatari za saratani Unywaji wa juisi ya tango hupunguza hatari ya saratani kwa wanawake hasa saratani...
Replies
7
Views
238
Tofali la kuchoma Hili ni tofali linalopatikana baada ya kutengeneza tofali la udongo na kulichoma kwa kutumia moto. Tanuri ya matofali unafunikwa kwa gana la udongo nje na chini yake moto inawaka kwa siku 2 au 3. Kutengeneza matoli wa njia hii ina gharama zaidi laini matofali yaliyochomwa...
Replies
0
Views
267
- Kuwa na maisha kamili/ full. - Kufanya maamuzi haraka, haina aja ya kushirikisha mtu.. mfano umepata kazi inayo kutaka kuama mkoa nk - Imarisha kazi au biashara yako bila kizuizi chochote, - Ishi maisha kwa njia yako mwenyewe. - Ishi bila kushughulika na fujo za mtu yeyote. Ongeza zingine
Replies
21
Views
361
Watu wengi wameendelea kuzungumzia suala la maadili, hasa kwa vijana. Kwa mfano hili wimbi la panyarodi linaloendelea kutajwa kwa vitendo viovu, hii ni miongoni mwa sababu kubwa ya mmomonyoko wa maadili. Inaonekana dhahiri baadhi ya wazazi wameshindwa kutimiza jukumu la malezi ya watoto wao...
Replies
10
Views
177
Ndizi ni mojawapo ya tunda linalopendwa zaidi duniani, likiwa limesheheni vitamini na madini. Ziko faida kadhaa za kiafya za ndizi ambazo ni muhimu kwa mlaji kula tunda hili. Faida hizi ni pamoja na: 1: Inasawazisha maji ya mwili "homoni": ndizi ina kiasi kikubwa cha potasiamu na vitamini B6...
Replies
6
Views
213

Donations

Total amount
$0.00
Goal
$300.00
Back
Top