- Jun 4, 2023
- 7,609
- 26,404
- 113
Kuoga maji baridi
Ni jambo gani la kwanza linalokuja akilini unapofikiria juu ya kuoga baridi?Faida za kuoga maji ya baridi
Kwanza maji ya baridi hukufanya uchangamke, hili ni tofauti na maji ya moto.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Thrombosis Research Institute, watu wanaooga maji ya baridi wanaongeza uzalishaji wa seli nyeupe za damu.
Utafiti huu unaeleza kuwa kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha metaboli mwili unapojaribu kujipasha moto, ndipo seli hizi nyeupe ambazo hupambana na maradhi zinapozalishwa.
Kumbuka hata wakati wa kuoga maji baridi kasi ya upumuaji hubadilika na kukufanya kuongeza kiasi cha oksijeni mwilini.
Pia, hulainisha ngozi na nywele tofauti na ilivyo kwa maji ya moto ambayo huchubua ngozi, hasa kwa kuondoa mafuta laini yanayolinda ngozi na nywele na kuzifanya ziwe kavu.
Kuoga moto
Watu wengi hupendelea kutumia maji ya moto kuoga pale hali ya hewa inapobadilika na kuwa ya baridi au wakati mwingine mtu anaumwa hivyo anatumia maji ya moto.Lakini kwa ajili ya urembo na afya ya ngozi, maji ya moto yanatajwa kuwa ni kitu muhimu. Hizi hapa ni baadhi ya faida zitokanazo na matumizi ya maji ya moto angalau mara tatu kwa wiki
Kulainisha na kutunza ngozi: Maji ya moto husaidia kulainisha ngozi yako tofauti na ukitumia maji ya baridi. Maji ya moto hasa yaliyo katika jakuzi ambapo utatumia muda mrefu kidogo ngozi yako ikiwa kwenye maji, husaidia kuilainisha ngozi yako na kuiweka katika hali nzuri.
Usingizi: Kama huwa unapata matatizo kupata usingizi usiku, amka oga kwa kutumia maji ya moto kwani husaidia kulainisha misuli ya mwili wako na itakaa sawa na utaweza kupata usinngizi.
Kukuweka katika hali nzuri: Kuna wakati mwingine mtu hujisikia uchovu wa mwili na kutotaka kufanya chochote (Off mood). Ukioga kwa maji ya moto yatakusaida kukuondolea uchovu na utajisikia mwenye nguvu na upo tayari kukabiliana na changamoto za siku.
Kuchangamsha ubongo: Unapooga kwa kutumia maji ya moto husaidia kuchangamsha ubongo na kuufanya uweze kufanyakazi kwa ufanisi na kwa haraka zaidi.
Kushusha shinikizo la damu: Ukiachanna na masuala ya urembo, kuoga maji ya moto kunatajwa kuwa ni njia ya haraka ya kusaidia kushusha shinikizo la damu. Tafiti zinaonyesha kuwa mtu mwenye shinikizo la damu la kupanda, akioga kwa maji ya moto husaidia kushusha.
Kusaidia mzunguko wa damu: Ukioga kwa kutumia maji ya moto husaidia kusisimu na kuitanua mishipa ya damu hivyo kuwezesha damu kuwa na mzunguko mzuri mwilini.
Unapendelea kuoga maji ya moto au baridi?