- Jun 4, 2023
- 7,609
- 26,404
- 113
Wahenga Walisema AKIBA HAIOZI.
Simamia matumizi bora ya fedha zako, kujenga maisha yako. Kuweka akiba ni moja ya matumizi mazuri ya kuhifadhi fedha yako. Wengi hudhania kuweka akiba ni lazima uwe na kipato kikubwa, lakini ukweli ni kwamba kuweka akiba ni maamuzi.
Weka angalau 5% - 40% kwenye akiba.
Wataalamu wanapendekeza kwamba hazina hii ya dharura (akiba) iwe sawa mara tatu au sita ya mshahara wako wa kila mwezi, kwa sababu ni bima ya kibinafsi ikiwa utapoteza kazi yako au kukabiliwa na gharama za afya zisizotarajiwa.
Mfano.
Kila siku unatenga Tsh.1000 au Tsh.5000/ au 10000/
Au unapanga kwamba kila wiki utaweka akiba ya Tsh.10,000/ au Tsh.50,000/= Au Tsh.100,000/
Hii itakusaidia kujizatiti (commitment) katika uwekaji wa akiba. Maana mfumo uliozoeleka na unaosisitizwa wa kuweka akiba ni kutenga asilimia 10% au 20% ya kila pesa unayopata.
Epuka matumizi yasiyo na lazima
Wengi wetu tuna matumizi yasiyo na lazima ambayo yanatupotezea mda na fedha kila siku.
Katika matumizi yako angalia matumizi yapi ambayo yanakigjarimu fedha na hayana ulazima. Matumizi haya yaache kabisa ili uweze kuongeza kipato chako cha akiba.
Tumia kiasi kidogo kwenye matumizi yasiyo ya msingi
Kuna matumizi mengi ambayo sio ya msingu mfano unakuta mtu anapitia sehemu anakula mishikaki akiwa anaelekea nyumbani, wakati huko nyumbani teyari kuna nyama. Tumia pesa kidogo kwa bidhaa ambazo hazichangii kwa kuishi kwako.
Kujenga mazoea ya kuishi kwa kipato chako
Kwa kawaida, tabia/mazoea yako hutengenezwa hasa na kipato chako. Watu wanaishi maisha ya gharama sana yasiyoendana na kipato Chao. Hapa unahitaji kuzingatia haswa nidhamu katika suala la matumizi ya fedha.
Jaribu kuishi kwa uchache wakati huu na usiwe na manunuzi ya kighafla. Baadaye siku za usoni, utagundua kuwa kutotumia pesnihovyo ni rahisi zaidi kuliko matumizi ya pesa ovyo.
Je unaweka akiba? njoo tujifunze kwa pamoja namna ya kuweka akiba.
Toa ushauri namna gani unaweza hifadhi akiba yako.
Simamia matumizi bora ya fedha zako, kujenga maisha yako. Kuweka akiba ni moja ya matumizi mazuri ya kuhifadhi fedha yako. Wengi hudhania kuweka akiba ni lazima uwe na kipato kikubwa, lakini ukweli ni kwamba kuweka akiba ni maamuzi.
Weka angalau 5% - 40% kwenye akiba.
Wataalamu wanapendekeza kwamba hazina hii ya dharura (akiba) iwe sawa mara tatu au sita ya mshahara wako wa kila mwezi, kwa sababu ni bima ya kibinafsi ikiwa utapoteza kazi yako au kukabiliwa na gharama za afya zisizotarajiwa.
Mfano.
Kila siku unatenga Tsh.1000 au Tsh.5000/ au 10000/
Au unapanga kwamba kila wiki utaweka akiba ya Tsh.10,000/ au Tsh.50,000/= Au Tsh.100,000/
Hii itakusaidia kujizatiti (commitment) katika uwekaji wa akiba. Maana mfumo uliozoeleka na unaosisitizwa wa kuweka akiba ni kutenga asilimia 10% au 20% ya kila pesa unayopata.
Epuka matumizi yasiyo na lazima
Wengi wetu tuna matumizi yasiyo na lazima ambayo yanatupotezea mda na fedha kila siku.
Katika matumizi yako angalia matumizi yapi ambayo yanakigjarimu fedha na hayana ulazima. Matumizi haya yaache kabisa ili uweze kuongeza kipato chako cha akiba.
Tumia kiasi kidogo kwenye matumizi yasiyo ya msingi
Kuna matumizi mengi ambayo sio ya msingu mfano unakuta mtu anapitia sehemu anakula mishikaki akiwa anaelekea nyumbani, wakati huko nyumbani teyari kuna nyama. Tumia pesa kidogo kwa bidhaa ambazo hazichangii kwa kuishi kwako.
Kujenga mazoea ya kuishi kwa kipato chako
Kwa kawaida, tabia/mazoea yako hutengenezwa hasa na kipato chako. Watu wanaishi maisha ya gharama sana yasiyoendana na kipato Chao. Hapa unahitaji kuzingatia haswa nidhamu katika suala la matumizi ya fedha.
Jaribu kuishi kwa uchache wakati huu na usiwe na manunuzi ya kighafla. Baadaye siku za usoni, utagundua kuwa kutotumia pesnihovyo ni rahisi zaidi kuliko matumizi ya pesa ovyo.
Je unaweka akiba? njoo tujifunze kwa pamoja namna ya kuweka akiba.
Toa ushauri namna gani unaweza hifadhi akiba yako.