- Joined
- Jun 4, 2023
- Messages
- 7,622
- Reaction score
- 26,437
- Points
- 113
Je, nini maana ya Urithi?
Urithi ni mali na madeni anayoacha mtu baada ya kifo chake kwa ajili ya watu ambao wanastahili kumiliki mali na madeni hayo kwa mujibu wa sheria
Nini lengo kuu la kuwapo sheria za Mirathi?
Lengo kuu la uwepo wa sheria za mirathi ni kuweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba mali na madeni ya marehemu vinasimamiwa kwa namna ambayo inazuia uwezekano wa kuhatarisha amani au kusababisha hasara kwa warithi wa marehemu na/au wadeni wake.
Ni sheria gani zinazosimamia masuala ya Mirathi Tanzania?
Hadhi na Imani ya marehemu wakati wa kifo chake ndiyo inayoamua Sheria gani itumike katika kushughulikia mirathi yake. Kwa ujumla, mojawapo ya, Sheria zifuatazo hutumika;
Je, ni mazingira gani ambayo yataamua matumizi ya Sheria husika ili kushughulikia mirathi?
Yapo mazingira ya aina mbili yanayoweza kuamua ni sheria gani itumike; Kwanza, pale ambapo mtu amefariki akiwa ameacha wosia, kile kilichoandikwa katika wosia ndicho kitakachoongoza mgawanyo wa mali na madeni yake, isipikuwa kama mahakama itashawishiwa kuamini vinginevyo. Pili, pale ambapo mtu amefariki bila kuandika wosia, kwa kuzingatia aina ya maisha aliyokuwa anaishi, mirathi yake itashughulikiwa kwa namna hiyo. Kwa mfano, kama marehemu aliishi kwa utamaduni na taratibu za kiislam, Sheria ya Kiislam kuhusu Mirathi itatumika.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya serikali huchukua mfumo upi?
Mgawanyo wa mali kwa sheria ya serikali huwa kama ifuatavyo;
Je, mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi?
Mtoto wa nje ya ndoa hana haki ya kurithi, isipokuwa tu kama ametajwa na kugawiwa fungu katika wosia wa marehemu.
Je, sheria ya kimila inatumika katika mazingira gani?
Sheria ya kimila hutumika kwa mtu ambaye wakati wa maisha yake aliishi kwa mujibu wa mila na desturi za kabila fulani, na hakuandika wosia kabla ya kifo chake.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya kimila huchukua mfumo upi?
Katika makabila yaliyo mengi Tanzania, ambayo hufuata mkondo wa kiume (patrilineal) mali za marehemu hugawanywa kwa kufuata upande wa ukoo wa kiumeni na warithi huwa ni watu wanaoangukia katika vyeo vya aina tatu ambavyo ni daraja la kwanza, daraja la pili na daraja la tatu.
Je, mjane ana nafasi gani katika sheria ya mila?
Sheria ya kimila katika tangazo la serikali namba 436 la mwaka 1963 haimruhusu mjane kurithi mali za marehemu mume wake. Mjane mwenye watoto inabidi aishi kwa kutegemea watoto wake. Mjane ambaye hana watoto atabaki katika nyumba ya marehemu na kupewa asilimia 20 ya nusu ya mali ya marehemu na kuitumia wakati wa uhai wake, akifariki au akiolewa na mtu mwingine nje ya ukoo wa marehemu mali hiyo na nyumba aliyokua anakaa hugawiwa kwa warithi halali wa marehemu mume wake.
Je, kwa mujibu wa sheria ya mila, mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi?
Sheria ya mila inatamka kua, watoto waliozaliwa nje ya ndoa hawaruhusiwi kurithi isipokua tu pale marehemu anapoacha wosia unaowapa haki ya kurithi au, Ikiwa walihalalishwa na marehemu kabla ya kufa.
Je, mwanamke anaweza kurithi ardhi chini ya sheria ya mila?
Sheria ya ardhi ya vijijini namba 5 ya mwaka 1999 imesahihisha utaratibu wa umiliki ardhi wa kimila (urithi wa ardhi) kwa kuondoa ubaguzi wa aina yoyote kwenye umiliki wa ardhi na kuweka usawa kwa wanawake na wanaume. Kwa misingi hii, cheo cha tatu cha urithi kwenye sheria za kimila kinakua batili pale urithi wa mali ya marehemu unapogusia suala la ardhi.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya kiislamu huzingatia mambo yapi?
Mgawanyo wa mali kwa sheria ya kiislamu huzingatia mambo yafuatayo;
Urithi ni mali na madeni anayoacha mtu baada ya kifo chake kwa ajili ya watu ambao wanastahili kumiliki mali na madeni hayo kwa mujibu wa sheria
Nini lengo kuu la kuwapo sheria za Mirathi?
Lengo kuu la uwepo wa sheria za mirathi ni kuweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba mali na madeni ya marehemu vinasimamiwa kwa namna ambayo inazuia uwezekano wa kuhatarisha amani au kusababisha hasara kwa warithi wa marehemu na/au wadeni wake.
Ni sheria gani zinazosimamia masuala ya Mirathi Tanzania?
Hadhi na Imani ya marehemu wakati wa kifo chake ndiyo inayoamua Sheria gani itumike katika kushughulikia mirathi yake. Kwa ujumla, mojawapo ya, Sheria zifuatazo hutumika;
- Sheria ya serikali
- Sheria ya Kimila
- Sheria ya dini ya kiislamu kuhusu mirathi
Je, ni mazingira gani ambayo yataamua matumizi ya Sheria husika ili kushughulikia mirathi?
Yapo mazingira ya aina mbili yanayoweza kuamua ni sheria gani itumike; Kwanza, pale ambapo mtu amefariki akiwa ameacha wosia, kile kilichoandikwa katika wosia ndicho kitakachoongoza mgawanyo wa mali na madeni yake, isipikuwa kama mahakama itashawishiwa kuamini vinginevyo. Pili, pale ambapo mtu amefariki bila kuandika wosia, kwa kuzingatia aina ya maisha aliyokuwa anaishi, mirathi yake itashughulikiwa kwa namna hiyo. Kwa mfano, kama marehemu aliishi kwa utamaduni na taratibu za kiislam, Sheria ya Kiislam kuhusu Mirathi itatumika.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya serikali huchukua mfumo upi?
Mgawanyo wa mali kwa sheria ya serikali huwa kama ifuatavyo;
- Kama marehemu ameacha mjane na watoto, mjane atapata ya mali zote za marehemu na watoto watapata ya mali zote za marehemu.
- Kama marehemu hakuacha watoto, mjane atapata nusu ya mali zote za marehemu na nusu nyingine hugawanywa sawasawa kati ya wazazi, kaka na dada za marehemu.
Je, mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi?
Mtoto wa nje ya ndoa hana haki ya kurithi, isipokuwa tu kama ametajwa na kugawiwa fungu katika wosia wa marehemu.
Je, sheria ya kimila inatumika katika mazingira gani?
Sheria ya kimila hutumika kwa mtu ambaye wakati wa maisha yake aliishi kwa mujibu wa mila na desturi za kabila fulani, na hakuandika wosia kabla ya kifo chake.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya kimila huchukua mfumo upi?
Katika makabila yaliyo mengi Tanzania, ambayo hufuata mkondo wa kiume (patrilineal) mali za marehemu hugawanywa kwa kufuata upande wa ukoo wa kiumeni na warithi huwa ni watu wanaoangukia katika vyeo vya aina tatu ambavyo ni daraja la kwanza, daraja la pili na daraja la tatu.
- Daraja la kwanza: Cheo hiki hushikiliwa na mtoto wa kwanza wa kiume kutoka katika nyumba ya kwanza (kama ilikuwa ndoa ya wake wengi) au mtoto wa kiume aliyezaliwa kwanza kutoka nyumba yoyote iwapo marehemu hakuacha mtoto wa kiume katika nyumba ya kwanza.
- Daraja la pili: Cheo hiki hushikiliwa na watoto wa kiume waliosalia ambao hurithi sehemu kubwa kuliko watoto wa kike ambao huhesabika kama daraja la tatu.
- Daraja la tatu: Cheo hiki ndio cha mwisho na kinajumuisha watoto wa kike bila kujali tofauti ya umri na nafasi ya mama zao katika ndoa. Daraja hili hupata sehemu ndogo kuliko watoto wa kiume na kama watoto wa kiume hawapo basi watoto wa kike huongezewa Urithi
Je, mjane ana nafasi gani katika sheria ya mila?
Sheria ya kimila katika tangazo la serikali namba 436 la mwaka 1963 haimruhusu mjane kurithi mali za marehemu mume wake. Mjane mwenye watoto inabidi aishi kwa kutegemea watoto wake. Mjane ambaye hana watoto atabaki katika nyumba ya marehemu na kupewa asilimia 20 ya nusu ya mali ya marehemu na kuitumia wakati wa uhai wake, akifariki au akiolewa na mtu mwingine nje ya ukoo wa marehemu mali hiyo na nyumba aliyokua anakaa hugawiwa kwa warithi halali wa marehemu mume wake.
Je, kwa mujibu wa sheria ya mila, mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi?
Sheria ya mila inatamka kua, watoto waliozaliwa nje ya ndoa hawaruhusiwi kurithi isipokua tu pale marehemu anapoacha wosia unaowapa haki ya kurithi au, Ikiwa walihalalishwa na marehemu kabla ya kufa.
Je, mwanamke anaweza kurithi ardhi chini ya sheria ya mila?
Sheria ya ardhi ya vijijini namba 5 ya mwaka 1999 imesahihisha utaratibu wa umiliki ardhi wa kimila (urithi wa ardhi) kwa kuondoa ubaguzi wa aina yoyote kwenye umiliki wa ardhi na kuweka usawa kwa wanawake na wanaume. Kwa misingi hii, cheo cha tatu cha urithi kwenye sheria za kimila kinakua batili pale urithi wa mali ya marehemu unapogusia suala la ardhi.
Je, mgawanyo wa mali kwa kutumia sheria ya kiislamu huzingatia mambo yapi?
Mgawanyo wa mali kwa sheria ya kiislamu huzingatia mambo yafuatayo;
- Sharti ithibitike kwamba mwenye mali ameshafariki (maut-al-muwarith)
- Kuwepo na warithi halali wa marehemu, yaani watoto wa marehemu na ndugu wengine na wote wawe warithi hakika wanaotambulika kisheria wakati wa mauti ya marehemu. (hayat-al-warith)
- Marehemu awe ameacha mali
- Urithi utokane na mali halisi na halali za marehemu