- Jul 3, 2023
- 1,897
- 3,986
- 113
Kipindi niko Moshi Kilimamjaro nilishangaa sana kukuta madukani hawauzi mkate nusu, kwanza muuza duka alinishangaa naulizia mkate nusu ikabidi ni nunue mkate mzimaa.
Leo nimepeleka zangu oda ya kuku, nikakutana na mtoto ametumwa sukari ya mia tatu, analia barabara nzima asaidiwe maana ameimwaga bahati mbaya hawezi rudi nyumbani atachapwa.
Nikajiuliza hii sukari ya mia tatu ikoje? au ni ile sukari guru? ndio wakaniambia ni sukari ya kawaida inauzwa vijiko viwili mia. Nilishangaa sana, ilibidi nimpe yule dogo jero maana bodaboda walikua wanamcheka hawa msaidii
Sikutegemea kama kuna mitaa inaweza uza sukari kwa kijiko ndio mara ya kwanza duniani nimelijua hili, ila yote kwa yote maisha yanasonga.
Mtaa unaokaa wanauza sukari kwa kijiko?, au wenzangu mnakaa udhuuunguni?
Leo nimepeleka zangu oda ya kuku, nikakutana na mtoto ametumwa sukari ya mia tatu, analia barabara nzima asaidiwe maana ameimwaga bahati mbaya hawezi rudi nyumbani atachapwa.
Nikajiuliza hii sukari ya mia tatu ikoje? au ni ile sukari guru? ndio wakaniambia ni sukari ya kawaida inauzwa vijiko viwili mia. Nilishangaa sana, ilibidi nimpe yule dogo jero maana bodaboda walikua wanamcheka hawa msaidii
Sikutegemea kama kuna mitaa inaweza uza sukari kwa kijiko ndio mara ya kwanza duniani nimelijua hili, ila yote kwa yote maisha yanasonga.
Mtaa unaokaa wanauza sukari kwa kijiko?, au wenzangu mnakaa udhuuunguni?