Jamii fulani za kasuku wanaweza kuishi miaka mia moja hivi, hata hivyo, ni vigumu sana kwa panya kuishi kwa zaidi ya miaka mitatu. Tofauti hiyo kubwa ya muda ambao viumbe huishi imefanya wanabiolojia fulani wakate kauli kwamba kuzeeka husababishwa na jambo fulani, na kama ni hivyo, basi huenda kukawa na tiba.
Kampuni nyingi za kutengeneza dawa zimetumia pesa nyingi kutafuta tiba inayofaa ya kuzuia kuzeeka. Isitoshe, hangaiko kuu la watu waliozaliwa baada ya Vita vya Pili vya Ulimwengu ambao sasa wana miaka 60 na kitu, limekuwa kutafuta dawa ya kuzuia kuzeeka.
Pia utafiti kuhusu kuzeeka umekuwa jambo kuu kwa wataalamu wengi wanaochunguza chembe za urithi, molekuli, wanyama, na kuzeeka na athari zake. Kitabu Why We Age, cha Steven Austad, kinasema: “Siku hizi kunakuwa na msisimko mwingi wataalamu wanaochunguza kuzeeka na athari zake