- Joined
- Jun 5, 2023
- Messages
- 26
- Reaction score
- 57
- Points
- 0
Kilabu kilianzishwa kikijulikana kama Newton Heath L & YR F.C. mwaka wa 1878 kama timu ya kazi ya bohari la Reli la Lancashire na Yorkshire huko Newton Heath. Mashati ya kilabu hiyo yalikuwa ya kijani na nusu dhahabu. Walicheza kwenye uwanja mdogo, uliochakaa huko North Road kwa miaka kumi na mitano, kabla ya kuhamia Bank Street katika mji wa karibu wa Clayton mwaka wa 1893. Kilabu kilikuwa kimeingia ligi ya kandanda ya Football Leagu mwaka uliotangulia na kuanza kukatiza uhusiano wake na bohari la reli, na ikawa kampuni ya kujitegemea, ikimteua katibu wa kilabu na kudondoasha herufi “L&YR” kutoka jina lao na kujiita Newton Heath F.C. Muda mrefu haukupita, mwaka 1902, kilabu kilikaribia kufilisika, kikawa na madeni ya zaidi ya £2,500. Wakati mmoja, uwanja wao wa Bank Street ulifungwa na wadai wao.[8]
Kabla ya kufungwa kabisa, kilabu kilipokea uwekezaji mkubwa kutoka kwa J. H. Davies, mkurugenzi mtendaji wa Manchester Breweries.[9] Kuna tetesi kuwa Harry Stafford, nahodha wa kilabu alikuwa akijivunia mbwa wake wa thamani wa aina ya St. Bernard katika mkutano wa kuchangishia kilabu fedha, wakati Davies alipomwendea ili kumnunua mbwa huyo. Stafford alikataa, lakini aliweza kumshawishi Davies kuwekeza katika kilabu na kuwa mwenyekiti wake.[10] Iliamuliwa katika kikao cha bodi ya mapema kuwa kilabu kilihitaji kubadilishwa jina ili kuashiria mwanzo huo mpya. Manchester Central na Manchester Celtic ni miongoni mwa majina yaliopendekezwa kabla ya Louis Rocca, mhamiaji mchanga kutoka Italy aliposema "Ndugu zangu, mbona tusijiite Manchester united?"[11] Jina hilo lilibakia hivyo, na Manchester United likawa jina rasmi tarehe 26 Aprili 1902. Davies pia aliamua itakuwa vyema kubadili rangi za kilabu, walitupilia mbalirangi za kijani na nusu dhahabu za Newton Health na kuchagua nyekundu na nyeupe kuwa rangi za Manchester United
Wikipedia
Kabla ya kufungwa kabisa, kilabu kilipokea uwekezaji mkubwa kutoka kwa J. H. Davies, mkurugenzi mtendaji wa Manchester Breweries.[9] Kuna tetesi kuwa Harry Stafford, nahodha wa kilabu alikuwa akijivunia mbwa wake wa thamani wa aina ya St. Bernard katika mkutano wa kuchangishia kilabu fedha, wakati Davies alipomwendea ili kumnunua mbwa huyo. Stafford alikataa, lakini aliweza kumshawishi Davies kuwekeza katika kilabu na kuwa mwenyekiti wake.[10] Iliamuliwa katika kikao cha bodi ya mapema kuwa kilabu kilihitaji kubadilishwa jina ili kuashiria mwanzo huo mpya. Manchester Central na Manchester Celtic ni miongoni mwa majina yaliopendekezwa kabla ya Louis Rocca, mhamiaji mchanga kutoka Italy aliposema "Ndugu zangu, mbona tusijiite Manchester united?"[11] Jina hilo lilibakia hivyo, na Manchester United likawa jina rasmi tarehe 26 Aprili 1902. Davies pia aliamua itakuwa vyema kubadili rangi za kilabu, walitupilia mbalirangi za kijani na nusu dhahabu za Newton Health na kuchagua nyekundu na nyeupe kuwa rangi za Manchester United
Wikipedia