Mkasa: Jinsi nilivyofundishwa uchawi

Welcome to our community

Looks like you don't have an account yet? Be apart of something great, join today! Create account to get more access like posting, reacting to others helpful post and your own private message Register Or Login

SEHEMU YA KWANZA.
Nikiwa nimerudi kutoka shuleni nilikutana na mama nje ambaye alinambia tumepata mgeni ambaye atakua akitusaidia kazi za ndani yaani dada wa kazi, kutokana na uchovu na fimbo za siku hio hata sikua na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu jambo hilo nilimjibu mama kwa kifupi.

“haya”. Huku nikielekea ndani ambapo nilifika na kumkuta dada mmoja aliyekua na umri kati na miaka kumi na saba hadi ishirini ambaye alinichangamkia kama mtu tuliyejuana siku nyingi.

“mambo clara habari ya shule”. Aliongea dada Yule. Na kunifanya nishangae kalijuaje jina langu lakini nilihisi huenda mama alishamwambia kwamba ana mtoto anaeitwa clara.

“nzuri shikamoo dada,”. Niimjibu kwa heshima kwa kua alikua ameninzidi ki umri hivyo alistahili heshima kwani mimi nilikua darasa la nne tu, baada ya kumjibu nilielekea ndani na kulitua begi langu pia nilikuta mizigo ya dada Yule ambaye ilionesha hakua amefika muda mrefu.

Kwakua tulikua tukipata chakula shuleni nilipitiliza kulala ambapo usingizi ulinipitia na nilikuja kustuka majira ya saa sita usiku ambapo nilimuona dada Yule akiwa ameketi kitandani uchi wa mnyama huku akiwa ameinguanisha mikono yake kama mtu aliyekua akisali.

Moyo wangu uliogopa sana na nililazimika kufikicha macho ili nijue kwamba ilikua ndoto au la na niligundua kwamba haikua ndoto bali ilikua ni ukweli kabisa.

Kisha dada Yule akasimama na kuanza kutembea tembea ndani ya chumba changu huku mikono akiwa ameikunja vile vile na macho yake yakiwa yamefungwa, na kisha baada ya muda, alirudi kitandani na kuketi kama alivyokua awali.

Baada ya dakika tano nilimshuhudia mama nae akija chumbani akiwa amevaa kama dada Yule, hapo nilishindwa kujizuia na kutamka.

“haaa, mama kumbe nawe mchawi”. Niliongea kwa mashangao kauli ambayo ilimstua sana mama na kisha akanisogelea bila uwoga na kuniambia.

“shhhhhhhhh, hakuna haja ya kujificha sasa mimi ni mchawi ndio na hata wewe ni lazima uwe mchawi au laa nikuue kama nilivyomfanya baba yako”.aiongea mama maneno ambayo yalinistua sana na kunifanya nianze kutetemeka.

“unaogopa nini? Mimi ni mchawi toka nilipokua na umri kama wewe umewahi kunigundua? Umewahi kuniona nikitisha? Acha ujinga mwanangu”. Aliongea mama na baada ya muda tulimshuhudia dada Yule wa kazi akiinuka huku macho yake yakiwa yanawaka kama tochi. Na hapo nilimshuhudia mama akipiga goti na kuanza kumsujudu dada Yule.

“naam mkuu, nimekuletea binti huyu akiwa kama mwanachama mpya”. Aliongea mama ambapo dada Yule alinitazama kwa makini sana kisha kumgeukia mama.

“inabidi tumfundishe taratibu kabla ya kumtambulisha kwa wenzetu”. Aliongea dada Yule kisha nilimshuhudia mama akiinuka na kunigeukia.

“mwanangu clara, wewe ndiye wa pekee kwangu na nimekuteua wewe upate kujua vitu vyangu vya ndani, na mbona sikuwaambia kaka zako? Naomba uniisitiri”. Aliongea mama na kunipa mtihani mgumu sana katika umri mdogo na mpaka apo sikua nimesema jambo lolote.

Mwisho mama alichukua unga mweupe na kunipaka katika paji la uso kisha tulijikuta sehemu nyingine kabisa ambayo ilikua ngeni kabisa lakini iionesha ilikua ni katika msitu uliopo kando ya barabara.

Kwani magari yalikua yakisikika yakipiita,
“mwanangu, huu ni msitu wa wachawi msitu ambao ukiingia kama si mchawi basi huwezi toka na utafanywa kafara”. Aliongea mama kauli ambayo ilinifanya niwaone wachawi ni watu wabaya.

“Watu wengi wamepotea katika msitu huu na vifo vyao vilikua vya kutatanisha , hiii ni kwasababu wanachukuliwa na mizimu na kufanywa kafara lakini mchawi si mtu mbaya ila wapo ambao wanautumia uchwi vibaya kwa kufanya visasi na mauaji”. Aliongea mama mambo mengi kuhusu uchawi kisha alinifundisha dawa nyingi sana za kichwawi ikiwemo za kupotea na kiini macho.

Kwakua muda ulikua umekwenda tulirejea nyumbani ambapo bado nilikua na maswali mengi sana na siku hio nilipanga ktoka na kwenda kwa rafiki yangu zuwena nipate kumuuliza mambo kadhaa kuhusu hali iliyonitokea jana usiku.

Nilimuaga mama vizuri na kumwambia nilikua nikienda kwa rafiki yang na alichonisisitiza ni kuwahi kurudi.
Nilipofika nyumbani kwa rafiki yangu kulikua kimya sana ambapo nilibisha hodi mara tatu na kufunguliwa na zuwena mwenyewe
“mambo clara”. Alinisalimu zuwena huku akinikaribisha ndani ambapo tulipiga storiza hapa na pale mwisho niliamua kumuuliza swali.

“eti unawafahamu wachawi”. Nilihoji
“eee, ni wanatisha sana na ni wabaya, wauaji na hawana huruma”. Zuwena aliongea kana kwamba ni mtu anaejua mambo mengi sana kuhusu uchawi.

“basi nikwambie kitu zuwena, mwenzio mama yangu ni……”. Kabla sijamaliza ilikuja sauti kichwani mwangu ambayo niliitambua kwamba ni ya mama.

“clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
 

Similar threads

  • Article Article
MWANZO Huu ni mkasa wangu ulionikuta baada ya kuhamishwa kutoka kigoma to dar es salaam early 2004s Baada ya kumaliza kazi zangu za kila siku ni kawaida yangu kutembelea kijiwe kwaajili ya kupata mawili matatu kutoka kwa watu mbalimbali wa rika tofauti lengo ni kutokua mpweke pia ku refresh...
Replies
60
Views
2K
Papa Francis amewaruhusu mapadre kuwabariki wapenzi wa jinsi moja, yakiwa ni maendeleo makubwa kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja na mahusiano mengine ya kijinsia wanaofahamika kama LGBT katika Kanisa Katoliki la Roma. Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki la Roma amesema makasisi wanapaswa...
Replies
9
Views
281
habari zenu hii ni true story by manenge. leo nimeona niwape japo kwa kirefu sana kuhusu hii kazi yangu ya professional tour guide,kwa majina yangu nileyepewa na wazazi wangu naitwa raymond joseph mushi,nimzaliwa wa machame. nimeona ni share nanyi ilimjue kuhusu hii kazi ambayo haina...
Replies
43
Views
1K
JINSI YA KUREJESHA KWA KUPAKA RANGI CHUPA ZA KIOO Chupa za kioo (glass) ziko za aina nyingi, zenye rangi, na ambazo hazina rangi yaani (transparent). Chupa hizi mara nyingi huwa ni mabaki/uchafu (trash) baada ya kutumia vilivyo ndani kama jibini, soda, bia, juice, mafuta, unga, asali au...
Replies
10
Views
696
Kusanya vipande vya sabuni Ni bora kutumia sabuni isiyo na harufu; kwa njia hii, unaweza kuongeza harufu yako mwenyewe. Ikiwa unataka kutumia sabuni yenye harufu nzuri, hakikisha kwamba mabaki yote yana harufu sawa, vinginevyo unaweza kuishia na mchanganyiko wa harufu mbaya. Ikiwa unataka...
Replies
6
Views
506

Donations

Total amount
$0.00
Goal
$300.00
Back
Top Bottom