- Jun 26, 2023
- 636
- 1,321
- 0
KITU NACHOTAKA BABA NINAHITAJI KUSOMA
Hodi hodi naingia, baba bora umekuja
kuna jambo kukwambia, nisikize mara moja
shairi nakusomea, sikiliza zangu hoja
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
wala 'sinipe kibaba, na shamba la kulima
eti unipe mbaba, na ndoa ya mapema
so niishie la saba, itanikuta nakama
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
sitaki watu kukaba, wala kwa watu kulima
eti mbeba kiroba, na kuwa mtu wa njama
sitaki kuwa kahaba, niwe wa nyumbani mama
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
sihitaji lako shamba, na mbuzi wako bandani
wala usinipe mavumba, sivitaki asilani
ukitaka mi kutamba, nipeleke tu shuleni
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
elimu kiniachia, kamwe haitaondoka
pesa zitaniishia, naweza kufirisika
mbuzi wataniibia, mashamba yatauzika
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
baba yangu mi mwanao, naomba nisikilize
sitaki yako makao, na tena usipuuze
shika nisemayo leo, kwenye kichwa uyatunze
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
niache tu napambana, baba nipe mahitaji
utafanya cha maana, utakuwa mwekezaji
vilabuni utajivuna, hawatakunywa maji
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
niweze jitegemea, nifanikiwe chuoni
utapata manufaa, utajua tu mbeleni
ufukara kuzuia, kuondoa maishani
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
kama kweli wanipenda, elimu weka ya kwanza
iwe moshi na mpanda, na usukumani mwanza
popote nitakapoenda, elimu itanitunza
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
baba leo ukienda, kwa Mungu kitangulia
malengo niliyounda, nani tanitimizia
sio nasema napenda, hebu jaribu fikiria
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
basi niachie mali, mbayo haiathiriwi
mali hiyo ni daftari, mali hiyo hailiwi
hii ni kubwa siri, wengi wao hawajuwi
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
leo hapa naishia, siwezi kuendelea
ukweli nimekuambia, ujumbe mekufikia
baba nakutegemea, elimu yangu simamia
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
Fanya ufanyavyo usiruhusu ujinga utawale ndani ya nyumba yako somesha watoto wako
Hodi hodi naingia, baba bora umekuja
kuna jambo kukwambia, nisikize mara moja
shairi nakusomea, sikiliza zangu hoja
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
wala 'sinipe kibaba, na shamba la kulima
eti unipe mbaba, na ndoa ya mapema
so niishie la saba, itanikuta nakama
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
sitaki watu kukaba, wala kwa watu kulima
eti mbeba kiroba, na kuwa mtu wa njama
sitaki kuwa kahaba, niwe wa nyumbani mama
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
sihitaji lako shamba, na mbuzi wako bandani
wala usinipe mavumba, sivitaki asilani
ukitaka mi kutamba, nipeleke tu shuleni
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
elimu kiniachia, kamwe haitaondoka
pesa zitaniishia, naweza kufirisika
mbuzi wataniibia, mashamba yatauzika
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
baba yangu mi mwanao, naomba nisikilize
sitaki yako makao, na tena usipuuze
shika nisemayo leo, kwenye kichwa uyatunze
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
niache tu napambana, baba nipe mahitaji
utafanya cha maana, utakuwa mwekezaji
vilabuni utajivuna, hawatakunywa maji
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
niweze jitegemea, nifanikiwe chuoni
utapata manufaa, utajua tu mbeleni
ufukara kuzuia, kuondoa maishani
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
kama kweli wanipenda, elimu weka ya kwanza
iwe moshi na mpanda, na usukumani mwanza
popote nitakapoenda, elimu itanitunza
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
baba leo ukienda, kwa Mungu kitangulia
malengo niliyounda, nani tanitimizia
sio nasema napenda, hebu jaribu fikiria
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
basi niachie mali, mbayo haiathiriwi
mali hiyo ni daftari, mali hiyo hailiwi
hii ni kubwa siri, wengi wao hawajuwi
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
leo hapa naishia, siwezi kuendelea
ukweli nimekuambia, ujumbe mekufikia
baba nakutegemea, elimu yangu simamia
kitu nachotaka baba, ninahitaji kusoma
Fanya ufanyavyo usiruhusu ujinga utawale ndani ya nyumba yako somesha watoto wako