Kwanini siamini kwamba Mungu yupo.....

Welcome to our community

Looks like you don't have an account yet? Be apart of something great, join today! Create account to get more access like posting, reacting to others helpful post and your own private message Register Or Login

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Mniwie radhi sina mpangilio naandika kadri vinavyokuja kichwani....

1. uovu wa bure (uovu usio na lengo)
Inajulikana kwamba yote yanayotokea hapa duniani, mazuri kwa mabaya, yamepangwa na Mungu.... yanatokea kwa sababu. Lakini kuna mambo mengi mabaya yasiofafanulika yanayotokea kwa watu wasio na hatia kabisa.... mfano, matetemeko ya ardhi, mafuriko.... yanauwa watu wengi ikiwemo watoto wadogo kabisa wasio na hatia. Nini hasa lengo la haya kutokea?? Mungu mwenye upendo analeta watu duniani ili wateseke??

2. Miungu inafanana na tamaduni zinazowaabudu
Kwakua Mungu ndie muumba wa ulimwengu basi anapaswa asiwe na ubaguzi wowote ule, ajulikane na viumbe wake wote. Kwa sasa kuna dini zaidi ya 4000 duniani.... kila dini na mungu/miungu yake. Kila dini inaamini mungu/miungu yake ndo imeumba ulimwengu. Lakini angalia.... tuchukulie mfano dini ya kikristo na mungu wake, Yahweh. Hii dini inaamini kwamba Yahweh ndiye muumba wa watu wote, lakini hata ukisoma vitabu vyake, matukio yote yanatokea kwenye sehemu za uarabuni na mediterranean, ambapo dini hii imezaliwa. Kwanini huyu Yahweh hakuhusiana na watu wa asia, africa na pengineko??

Miungu inafanana na tamaduni zilizowatengeza, 'gods are a reflection of the cultures that created them' watu wakiushaunganika na kuunda jamii, watakua na maswali 'tumetoka wapi??' 'jua linawakaje??' 'mtu akifa anaenda wapi??' kwahiyo wanatengeneza miungu na kuipa nguvu kwenye fikra zao, ya kujibu haya maswali, na pia kutengeneza mifumo ya sheria za kuongoza watu. Angalia jinsi ambavyo dini nyingi zinakaa kwenye upande wa kukandamiza wanawake. Ni kwasababu tamaduni za zamani zilikua hivyo, na miungu ikatengenezwa kuendana na hali hiyo, miungu ilitumika kama mfumo wa sheria....

3. Mbinguni na Kuzimu
Karibia dini zote zina sehemu mbili ambapo mtu anaenda baada ya kufa kulingana na matendo yake. Kuna mbinguni, sehemu wanayoenda wenye mazuri, na kuzimu, sehemu wanyoenda wenye mabaya. Na sehemu hizi ukienda ndo unabaki huko milele... Sasa tunatambua kwamba ili chochote kiwe na thamani, lazima kiwe na mwisho.... Maisha ni mazuri kwasababu yana mwisho.... Sasa iweje kuishi milele huku ukiungua, ama kusifu na kuabudu... hufanyi chochote kingine, ikawa ni kitu kizuri?? Jaribu kutafakari.... Labda kama unafanya hivyo, usiwe na akili uliyo nayo sasa yaani mungu akuondolee uwezo wako wa kuamua(free will)

4. Hofu ya Mungu
Tunajua kabisa kwamba mungu ndie muumba wa vyote, na mwenye mamlaka.... sasa kwanini atake kuogopwa na viumbe wake?? Kwanini?? Nguvu zote anazo yeye, lakini bado anataka umuogope, itamsaidia nini?? umsujudu na kumsifu, itamsaidia nini?? mtasema sababu zake hazijulikani lakini kwanini atawale kwa hofu, kwanini anahangaika sana na sisi viumbe wa chini?? Ukinywa pombe, ukizini, anakasirika.... kwanini?? ina maana anapata furaha kupitia hofu yetu.... je, ni kitu kizuri hiki?? anakupa uhuru wa kuamua, ila kuna vitu ukiamua anakasirika, huu ndo uhuru?? Jiulizeni maswali haya....

5. Kwanini hajidhihirishi??
Unadhani mungu angejidhihirisha kuna mtu angetia shaka juu ya uwepo wake?? kwa nini asijionyeshe wazi kabisa, macho ya damu na nyama yamuone ili aweze kupata uaminifu kutoka kwa wanadamu?? mtasema itaharibu uwezo wa kuchagua, lakini si anataka tumchague yeye?? akijionyesha wote si tutamchagua yeye??

zipo nyingi, ila ntazidi kuongezea kama kuna watu watauliza chochote. Acha niishie hapa....

@Gily
 

Hakimu

Immortal Village Hero
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 3, 2023
Messages
2,711
Reaction score
6,226
Points
113
Kwanza mbona wajachanganya kwamba mtu anafreewill pia kapangiwa (hii haiwezekani)

Mungu amempa kila mmoja uamuzi wa kuamua, niwachache sana ndio aliingilia maamuzi yao ili aonyesha jambo au kumuepusha kufanya kitu, au anaingilia maamuzi yake ili tu kwa sababu ya mtu mwingine apate ugumu au wepesi wa kufanya jambo

Japo kuwa na freewill yetu still he knows mpaka mwisho wetu, kwaiyo maisha yetu ni kama marudio ya filamu kwake ila kwa neema tu Mungu hatamwacha mtu afe asijue habari yake (kuamini ni kazi yako)

Soma
YEREMIA 3
Israeli asiye mwaminifu
1 Watu husema, Mtu akimwacha mkewe, naye akienda zake, akawa mke wa mtu mwingine, je! Mtu huyo atamrudia tena? Je! Nchi hiyo haitatiwa unajisi? Lakini wewe umefanya mambo ya ukahaba na wapenzi wengi; nawe, je! Utanirudia mimi? Asema BWANA. 2 Inua macho yako, ukavitazame vilele vya milima, ukaone; pako wapi mahali ambapo hawakulala nawe? Kando ya njia umeketi ili kuwangojea, kama vile Mwarabu jangwani; nawe umeitia nchi unajisi kwa ukahaba wako na uovu wako. 3 Kwa sababu hiyo manyunyu yamezuiliwa, wala hapakuwa na mvua ya vuli; hata hivyo ulikuwa na kipaji cha uso cha kahaba, ulikataa kutahayarika. 4 Je, tokea wakati huu hutanililia, Ee Baba yangu, wewe u kiongozi wa ujana wangu? 5Je! Ataishika hasira yake hata milele? Ataishika hata mwisho? Tazama, umesema hivyo, bali umetenda mambo mabaya, umefuata njia yako mwenyewe.
Mwito wa kutubu
6 Tena, BWANA akaniambia siku za mfalme Yosia, Je! Umeyaona aliyotenda Israeli mwenye kuasi? Amepanda juu ya kila mlima mrefu, akafanya huko mambo ya ukahaba, tena, chini ya kila mti wenye majani mabichi. 7 Nami nilisema baada ya yeye kuyatenda hayo yote, Atanirudia mimi, lakini hakurudi; na dada yake, Yuda mwenye hiana, akayaona hayo. 8 Nami nikaona, wakati nilipokuwa nimemwacha Israeli mwenye kuasi, nikampa hati ya talaka kwa sababu hiyo ya kuzini, dada yake, Yuda mwenye hiana, hakufanya hofu; bali yeye naye akaenda akafanya mambo ya ukahaba. 9Hata ikawa, kwa sababu alikuwa mwepesi wa kufanya ukahaba, nchi ikatiwa unajisi, naye akazini na mawe na miti. 10 Na pamoja na hayo yote dada yake, Yuda mwenye hiana, hajanirudia mimi kwa moyo wake wote, bali kwa unafiki, asema BWANA. 11BWANA, akaniambia, Israeli mwenye kuasi amejionesha kuwa mwenye haki kuliko Yuda mwenye hiana. 12 Nenda, ukatangaze maneno haya kuelekea upande wa kaskazini, ukaseme, Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi, asema BWANA; sitakutazama kwa hasira; maana mimi ni mwenye rehema, asema BWANA, sitashika hasira hata milele. 13 Ungama uovu wako tu

Lazima ujue Mungu anafanya kazi kwa kushawishi na kukuonyesha njia yake, na kwaneema sometimes huja mwenyewe, hua anabadilisha sana hatima zetu uliatupe nafasi ya mwisho kama unavyoona wanaisrael walikuwa wanafanya dhambi na Mungu alitulia tu akisubiri warudi kwake (freewill) ila baada ya kuona ndio wanazidi kukengeuka alibidi afanye jambo kuwaeleza uwepo wake ili kubadili hatima

Kuhusu kudhihirika kwa Mungu Anadhihirika Mungu ni roho, na hudhiirika kwa roho na matendo japo kwa need hata kwa macho pia
jaribu kufikia kiwangi fulani cha imani au kuonesha nia yeye atapatiliza

kuhusu kuwa Mungu anafata mila za jamiifulani alioanzisha sio kweli kwa ukristo, Tukianza kwa agano la kale Mungu ndiye aliyekuwa akiwapa sheria wanadamu na sheria nyingi zilikuwa tik for tat, ua uuliwe, zini upigwe mawe

Mungu yuleyule alikuja kuuleta upendo duniani kwa kuzaliwa, ilaaa kibinadamu huwezi zaliwa ulimwengu mzima ila kwa nguvu na neema zake, kotu tunamjua na anafanya kazi

dini ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu ila Wokovu ni mpango wa Mungu kumtafuta mwanadamu, dini hata wewe unaweza anzisha

Pia kuna shetani adui wa Mungu huyu yupo kupindisha kila kitu, yeye pia ataleta dini yake kudai unamwabudu Mungu kumbe sio atajaza mapepo ilimuone matendo kidogo ya kuridhisha, huyu ndie mpotoshaji mkuu

pia nafikiri kuwa Mungu licha ya kumuumba mwanadamu amuabudu pia alitaka kumonesha kuwa japo kuwa na nafasi yako ilivyokuwa mbinguni, ila kiumbe dhaifu kutoka kwenye udongo atanaweza kukushinda bila jasho kwa kunitegemea na kuninyenyekea tu, na hutakuwa na lakufanya

Moto uliumbwa kwa ajili ya shetani ila baada ya binadamu kukengeuka haina jinsi maana mbinguni hapaingii kilicho kichafu na hakuna sehemu nyingine, ila ukifa kabla ya siku ya hukumu mapepo kuzimu yatakutesa mpaka pale hukumu na utupwe motoni

Kuna andiko nitalitafuta ila silikumbuki linaonesha jinsi gani Mungu mwenye upendo na rehema pia anaupande mwingine wenye kutisha, pale watu watakavyo kuwa wanateseka yeye atacheka na kuwadhihaki
 

Gily

KF Founder & Dragon IGM
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 4, 2023
Messages
7,609
Reaction score
26,404
Points
113
Je swali, hapa duniani kuna vitu vingi vinatokeq ambavyo vina mkojo wa mwanadamu; mfano
1 Greenhouse gases emissions
2 Ukataji wa miti kiholela
3 Uharibifu wa mazingira nk

Mungu anahisikaje na uharibufu huu?
 

Gily

KF Founder & Dragon IGM
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 4, 2023
Messages
7,609
Reaction score
26,404
Points
113
Mniwie radhi sina mpangilio naandika kadri vinavyokuja kichwani....

1. uovu wa bure (uovu usio na lengo)
Inajulikana kwamba yote yanayotokea hapa duniani, mazuri kwa mabaya, yamepangwa na Mungu.... yanatokea kwa sababu. Lakini kuna mambo mengi mabaya yasiofafanulika yanayotokea kwa watu wasio na hatia kabisa.... mfano, matetemeko ya ardhi, mafuriko.... yanauwa watu wengi ikiwemo watoto wadogo kabisa wasio na hatia. Nini hasa lengo la haya kutokea?? Mungu mwenye upendo analeta watu duniani ili wateseke??

2. Miungu inafanana na tamaduni zinazowaabudu
Kwakua Mungu ndie muumba wa ulimwengu basi anapaswa asiwe na ubaguzi wowote ule, ajulikane na viumbe wake wote. Kwa sasa kuna dini zaidi ya 4000 duniani.... kila dini na mungu/miungu yake. Kila dini inaamini mungu/miungu yake ndo imeumba ulimwengu. Lakini angalia.... tuchukulie mfano dini ya kikristo na mungu wake, Yahweh. Hii dini inaamini kwamba Yahweh ndiye muumba wa watu wote, lakini hata ukisoma vitabu vyake, matukio yote yanatokea kwenye sehemu za uarabuni na mediterranean, ambapo dini hii imezaliwa. Kwanini huyu Yahweh hakuhusiana na watu wa asia, africa na pengineko??

Miungu inafanana na tamaduni zilizowatengeza, 'gods are a reflection of the cultures that created them' watu wakiushaunganika na kuunda jamii, watakua na maswali 'tumetoka wapi??' 'jua linawakaje??' 'mtu akifa anaenda wapi??' kwahiyo wanatengeneza miungu na kuipa nguvu kwenye fikra zao, ya kujibu haya maswali, na pia kutengeneza mifumo ya sheria za kuongoza watu. Angalia jinsi ambavyo dini nyingi zinakaa kwenye upande wa kukandamiza wanawake. Ni kwasababu tamaduni za zamani zilikua hivyo, na miungu ikatengenezwa kuendana na hali hiyo, miungu ilitumika kama mfumo wa sheria....

3. Mbinguni na Kuzimu
Karibia dini zote zina sehemu mbili ambapo mtu anaenda baada ya kufa kulingana na matendo yake. Kuna mbinguni, sehemu wanayoenda wenye mazuri, na kuzimu, sehemu wanyoenda wenye mabaya. Na sehemu hizi ukienda ndo unabaki huko milele... Sasa tunatambua kwamba ili chochote kiwe na thamani, lazima kiwe na mwisho.... Maisha ni mazuri kwasababu yana mwisho.... Sasa iweje kuishi milele huku ukiungua, ama kusifu na kuabudu... hufanyi chochote kingine, ikawa ni kitu kizuri?? Jaribu kutafakari.... Labda kama unafanya hivyo, usiwe na akili uliyo nayo sasa yaani mungu akuondolee uwezo wako wa kuamua(free will)

4. Hofu ya Mungu
Tunajua kabisa kwamba mungu ndie muumba wa vyote, na mwenye mamlaka.... sasa kwanini atake kuogopwa na viumbe wake?? Kwanini?? Nguvu zote anazo yeye, lakini bado anataka umuogope, itamsaidia nini?? umsujudu na kumsifu, itamsaidia nini?? mtasema sababu zake hazijulikani lakini kwanini atawale kwa hofu, kwanini anahangaika sana na sisi viumbe wa chini?? Ukinywa pombe, ukizini, anakasirika.... kwanini?? ina maana anapata furaha kupitia hofu yetu.... je, ni kitu kizuri hiki?? anakupa uhuru wa kuamua, ila kuna vitu ukiamua anakasirika, huu ndo uhuru?? Jiulizeni maswali haya....

5. Kwanini hajidhihirishi??
Unadhani mungu angejidhihirisha kuna mtu angetia shaka juu ya uwepo wake?? kwa nini asijionyeshe wazi kabisa, macho ya damu na nyama yamuone ili aweze kupata uaminifu kutoka kwa wanadamu?? mtasema itaharibu uwezo wa kuchagua, lakini si anataka tumchague yeye?? akijionyesha wote si tutamchagua yeye??

zipo nyingi, ila ntazidi kuongezea kama kuna watu watauliza chochote. Acha niishie hapa....

@Gily
Mungu anaweza kuwa amejifunua kwako. Je leo hii akaja kujifunua kwako utakubali kuwa Yeye ni Mungu?
 

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Huelewi wewe nini maana ya freewill siuamuzi binafsi wewe ukiamua kuua utakua na hatia mbele zake umeua, haingilii maamuzi ila kwa sababu
free will haina consequences, ni uhuru wa kuamua.... sasa unaambiwa uamue ila kuna kitu ukiamua unaadhibiwa, uhuru ukowapi??

huoni kama hizi ni falsafa za kizamani??
 

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Kejeli zipi tena? Nimeuliza kama madhara nasababisha mimi mwenyew inakuwaje utake Mungu aepushe?

Sijakataa pia kuwa kuna vitu hutokea na kama wanadamu vinatuumiza sana.
kwasababu mungu ni omnipotent, anaweza chochote

hivyo kwanini asitumie huu uweza wake kuzuia mabaya??
 

Gily

KF Founder & Dragon IGM
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 4, 2023
Messages
7,609
Reaction score
26,404
Points
113
kwasababu mungu ni omnipotent, anaweza chochote

hivyo kwanini asitumie huu uweza wake kuzuia mabaya??
Toka hapo mwanzo nimekuelewa. Sasa kama Mungu akiingilia kila jambo analifanya mwanadamu kutakuwa na free will?

Mfano wewe unapenda kula mbususu. Ikiwepo Mungu akazuiq usile mbususu kabisa kwa sababu unafanya nje ya mkataba wa ndoa. Hapo unaona sawa?
 

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Toka hapo mwanzo nimekuelewa. Sasa kama Mungu akiingilia kila jambo analifanya mwanadamu kutakuwa na free will?

Mfano wewe unapenda kula mbususu. Ikiwepo Mungu akazuiq usile mbususu kabisa kwa sababu unafanya nje ya mkataba wa ndoa. Hapo unaona sawa?
kwanini anichome moto sasa kama kweli nipo 'free'?? si nimeamua??

kwanini azunguke asiseme tu kwamba hiki hakiruhusiwi, adhabu yake ni hii...
 

Hakimu

Immortal Village Hero
KF Founder
KF Moderator
Joined
Jun 3, 2023
Messages
2,711
Reaction score
6,226
Points
113
watoto hawapewi free will wanapewa onyo
Mungu anampa freewill kila mwanadamu ndio maana kuna watoto hawajazaliwa lakini ni wachawi, wengine wana umri wa miezi 2- miaka 12 bado ni wachawi

Dogo ulimwengu wa roho upo tofauti roho hainaga utoto pale tu inapoingia kwenye mwili inauamuzi wake
 

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Mungu anampa freewill kila mwanadamu ndio maana kuna watoto hawajazaliwa lakini ni wachawi, wengine wana umri wa miezi 2- miaka 12 bado ni wachawi

Dogo ulimwengu wa roho upo tofauti roho hainaga utoto pale tu inapoingia kwenye mwili inauamuzi wake
sayansi inajaza magepu yote....

dhana za dini zitapotoka taratibu kadri tunavyozidi kuujua ulimwengu kwa upana wake, kitu ambacho hamna kitabu cha dini kinaweza kuelezea, vinaishia tu kusema juu ya anga ni mbinguni....
 

mshamba_mkuu

New member
Joined
Jun 4, 2023
Messages
1,563
Reaction score
4,525
Points
0
Sidhani kama hapa @Hakimu kakubali chunga sana we @mshamba_mkuu navyomjua anakuja kivingine 😬
ni ngumu sana kukubaliana kati ya theist na atheists, hapa nimeongea machache sana....

mi mwenyewe sikubadilishwa na mtu ilitokea tu yenyewe....

wanasema 'the best way to become an atheist is to read the bible with an open mind'
 

Similar threads

Wakuu kuuliza sio ujinga Hivi haya matairi yaliyo nyanyuliwa inakuwaga ni kwasababu gani maana nmejaribu kujiuliza Je niili yasichafuke? Au yanapancha? Au gari alina mzigo? Au linapunguza ulaji wamafuta? Au linatumika kama breki😄 Wadau mnisaidie, au yamechoka yanpokezana na wenzake kwa zamu?
Replies
7
Views
88
Niaje wakuu, hivi wabongo wanawazaga nini? Unakuta mtu anawazazi kijijini wakati wazazi wako hai hawajengei nyumba na hela ipo.. Ila mzazi akifa tu ndio anaanza kujenga kwa fujo(wiki moja), hizi hela za kujenga nyumba haraka hvi zinakuwaga wapi sku zote?.. Unajiuliza inamaana marehemu hakustaili...
Replies
7
Views
127
Daaah hii mada ngumu kumeza haina haja ya salamu... Kichwa chenyewe kokii. Lazima kikufikirishe pia kikupe uoga tuu. Tunaanza hiviii. Kifo ni ile hali ya uhai kutoka ndani ya kiumbe hai chochote. Kifo kinaweza kumtokea mtu, mnyama, bakteria, kirusi, mmea, jani n.k. Vyote hivi maadamu vina...
Replies
26
Views
286
Nina maana ukipata watu 20 au 30 kila siku mtu mmoja anatoa 5000 au 10000 na kila siku mtu mmoja anatoka. Siitatusaidia kidogo kupambana na maisha. Wewe ni prezidaa uwezi kimbia ukaacha app
Replies
102
Views
2K
Samaleko... Binafsi natumia Dolby perfume na Amara deodorant kwa sababu zinanukia vizuri na pia ni very affordable kwa majobless kama mimi. Wewe unatumia ipi? Share with us!
Replies
36
Views
700

Donations

Total amount
$0.00
Goal
$300.00
Back
Top Bottom